Skip to main content

RONALDO NA KASHFA KAMA YA MESSI

Unakumbuka ile kesi ambayo ilimkumba Lioneil Messi na mamlaka za mapato za nchini Hispania hadi akapigwa faini ya euro 2m pamoja na kifungo cha nje? sasa kesi ile imehamia kwa mpinzani mkubwa wa Messi ambaye ni Cristiano Ronaldo.

Taarifa zinasema kwa muda sasa toka mwaka 2011 hadi 2014 nyota huyo wa timu ya Real Madrid amekuwa akikwepa kulipa kodi ambapo zaidi ya kiasi cha kodi cha euro 14m amekwepa kulipa katika kipindi hicho.

Tofauti na Lioneil Messi lakini kwa Ronaldo kosa lake ni kubwa sana kwani wapelelezi wa kesi yake wanadai mshambuliaji huyo alifungua hadi kampuni kwa jina jipya ili kukwepa kulipa kodi na kiasi ambacho Ronaldo amekwepa ni mara 3 ya kile kilichomtia Lioneil Messi matatani.

Messi kesi yake ilikuwa ni ukwepaji wa kodi kiasi cha euro 4.1m huku Cristiano Ronaldo ikiwa ni euro 16m, na Messi na baba yake walihukumiwa adhabu ya miezi 21 na faini ya euro 2m hali inayoonesha Ronaldo anaweza kukabiliwa na adhabu kubwa zaidi.

Ronaldo mwenyewe akizungumzia tukio hilo nchini kwao Ureno alipoulizwa na waandishi wa habari alijibu “Quien no debe no teme” akimaanisha “asiye na kitu cha kuficha hawezi kuogopa chochote” na akisisitiza haogopi kitu na ana uhakika wa kushinda kesi hiyo.

Sheria za masuala ya kodi nchini Hispania zinaweza kumuokoa Ronaldo asiende jela kwani kama hujawahi kupata kesi ya kulipa kodi hapo mwanzo au hujawahi kwenda jela na ikiwa ni mara yako ya kwanza kupata kesi kama hiyo baasi unatumikia kifungo cha nje ya jela.

Comments

Popular posts from this blog

JEZI YA NYUMBANI YA BARCELONA MSIMU WA 2018/2019 IMEVUJA MTANDAONI

Hamza matwany Jezi ya barcelona ya msimu wa 18/19 ambayo inatengezwa na kampuni ya vifaa vya michezo vya nike imevuja mtandaoni. Jezi hiyo ambayo inafanana na jezi ambayo ilitumiwa na club hiyo mwaka 1998 miaka 20  nyuma imetengezwa katika namna hiyo ili kuenzi legends kwa klabu hiyo Jezi ya nyumbani itakuwa ina wekundu na mistari ya blue na bukta nyeusi pia socks zake ni nyeusi kama inavyoonekana kwenye hizo picha

UNYONGE WA ROMA ULIVYOWAPELEKA SEMI FINAL

Na Hamza matwany. Roma usiku wa tarehe 10/7/2018 ameweza kuushangaza ulimwengu kwa kile kitendo cha kumtoa fc Barcelona kwenye hatua ya robo fainali kwa kupindua matokeo ambapo mwanzoni alifungwa goli 4-1 nou camp na kufanikiw Kushinda goli 3-0 pale stadio olimpio jijini Roma. wapenzi wengi wa mchezo huu hawakumpa nafasi Roma kwenda hatua inayofuata katika michuano hii kwa sababu tu ndo timu pekee ilionekana kama dhaifu kwa timu zilizoingia hatua ya robo fainali. Roma ambae alipita kwa sharkter donestk kwa changamoto ya goli la ugenini lakini katika makundi alipita katika timu kama chelsea , Atletico Madrid na katika timu hizo kote alipata matokeo yaliyomsaidia kufika katika hatua hizi. Barcelona waliingia katika mchezo wakiwa na spirit ya kwamba mchezo umeisha toka nou camp ,walicheza kwa kujiamini kwamba hakuna maajabu yoyote yanaweza kutokea kwa vile tu walimchukulia kama mnyonge , huku wakiwa wamesahau kwamba hawajawahi kushinda katika stadio olimpio katika mechi 3 za mwisho a...

DUNIA YA SOCCER IMEJIFUNZA KITU.

Hamza matwany Usiku wa tarehe 10 &11-2018 ulikuwa moja ya siku ambazo timu kutoka SERIE A zimeonyesha kwamba mpira ni dakika 90 kwa mechi moja lakini ni 180 kwenye hatua ya mtoano hasa kwenye Champions league . Roma na juventus zilionekana timu ambazo mechi zao za marudiano zitakuwa rahisi kutokana na matokeo ambayo waliyapata mechi zao za kwanza Juve alipoteza mechi yake ya kwanza akiwa nyumbani kwa jumla ya goli 3-0 dhidi ya miamba ya jiji la madrid na Roma alifungwa 4-1 pale Nou camp. Mechi za marudio barcelona alimfuata Roma pale stadio olimpio na Roma alifanikiwa kupata ushindi wa goli 3-0 hivyo kufanya agg 4-4 na goli la ugenini lilimpa nafasi ya kusonga mbele. madrid alimkaribisha Juventus pale Stadio de bernabeu huku madrid wakimkosa naodha wake sergio ramos na Juventus wakimkosa paul dybala wote hao wakiwekwa nje kwa kadi. lakini juve aliusimamisha usiku kama Roma alivyofanya kwa kumfunga madrid goli 3-1 hivyo kufanya agg 4-3 , kitu ambacho hakikutazamwa na wengi kweny...