Skip to main content

KUELEKEA MCHEZO KATI YA PSG NA REAL MADRID

  Na Muller Idriss
Mnamo tar 11 Dec droo ya michuano ya klabu bingwa barani ulaya maarufu kama Uefa ilifanyika na moja kati ya mchezo ulioamsha hisia za wengi hususani wadau wa mchezo wa soka ni mchezo kati ya wababe wa ufaransa PSG dhidi ya Real Madrid.
Japo wengi wanautazama mchezo huu kwa kumpa PSG nafasi kubwa ya kushinda na wachache wakimpa Real Madrid kwa sababu ya historia yake kwenye michuano hii ya uefa.

Real madrid ndio mabingwa mara kumi na mbili katika michuano hii huku PSG wakiwa hawajawahi kupata ubingwa wa michuano  hii tangu kuanzishwa kwake.
   Hizi timu zimekutana mara 7 tangu kuanzishwa kwa hizi timu huku mara sita (6) kati ya hizo ikiwa ni michuano mbalimbali barani ulaya na mara moja ikiwa ni mechi ya kirafiki (pre_season)
Kwa mara ya kwanza timu hizi zilikutana msimu wa mwaka 1992/93 ambapo mchezo wa kwanza Madrid alishinda nyumbani kwa mabao 3_1 na waliporudi Ufaransa, wababe hao wa Hispania walikubali kupokea kichapo cha mabao 4_1 hivyo Real Madrid kuondolewa kwenye michuano hiyo.
   Mara ya tatu ni msimu wa mwaka 1994/1995 ambapo mchezo wa kwanza Real Madrid akiwa nyumbani alikubali kichapo cha bao moja kwa bila 1_0 kutoka kwa PSG na waliporudi Ufaransa mchezo ulimalizika kwa sare ya bila kufungana na kukamilisha jumla ya michezo minne.
    Mwaka 2015 timu hizo zilikutana katika michuano hii zikiwa zimepangwa kundi moja ambapo mchezo wa kwanza ulimalizika   kwa sare ya bila kufungana pale Ufaransa na waliporudi Hispania PSG walikubali kipigo cha bao moja kwa bila (1_0).
Na mara ya mwisho walikutana katika pre season mwaka 2016 na Real madrid ililazwa bao 3 kwa 1
Kwa ujumla wake PSG ameshinda michezo mitatu kati ya 7 waliyokutana na Real madrid akishinda michezo 2 kati ya hiyo 7 na wakitoka sare mara 2.
Ukiachana na Historia hizo tuje kuangalia perfomance ya timu hizi mbili kwa sasa..PSG wapo juu kwenye msimamo wa ligi huku Real madrid wakiwa katika nafasi ya tatu kwenye La liga. Safu ya ushambuliaji ya PSG ikiwajumlisha Neymar,Mbappe na Cavanni imefunga magoli 32 mpaka sasa kwenye league 1 huku ile ya Real Madrid Ronaldo,Isco na Asensio ikiwa imefunga magoli 12 tu kwenye La liga pia safu ya PSG imefunga magoli 16 kwenye Uefa mpka sas na madrid ikiwa imefunga magoli 12
Kwa upande wangu nautazama mchezo huu kama mchezo mmoja mzuri sana ambao dunia itashuhudia historia nyingine ikiwekwa katika soka barani ulaya

Comments

Popular posts from this blog

JEZI YA NYUMBANI YA BARCELONA MSIMU WA 2018/2019 IMEVUJA MTANDAONI

Hamza matwany Jezi ya barcelona ya msimu wa 18/19 ambayo inatengezwa na kampuni ya vifaa vya michezo vya nike imevuja mtandaoni. Jezi hiyo ambayo inafanana na jezi ambayo ilitumiwa na club hiyo mwaka 1998 miaka 20  nyuma imetengezwa katika namna hiyo ili kuenzi legends kwa klabu hiyo Jezi ya nyumbani itakuwa ina wekundu na mistari ya blue na bukta nyeusi pia socks zake ni nyeusi kama inavyoonekana kwenye hizo picha

UNYONGE WA ROMA ULIVYOWAPELEKA SEMI FINAL

Na Hamza matwany. Roma usiku wa tarehe 10/7/2018 ameweza kuushangaza ulimwengu kwa kile kitendo cha kumtoa fc Barcelona kwenye hatua ya robo fainali kwa kupindua matokeo ambapo mwanzoni alifungwa goli 4-1 nou camp na kufanikiw Kushinda goli 3-0 pale stadio olimpio jijini Roma. wapenzi wengi wa mchezo huu hawakumpa nafasi Roma kwenda hatua inayofuata katika michuano hii kwa sababu tu ndo timu pekee ilionekana kama dhaifu kwa timu zilizoingia hatua ya robo fainali. Roma ambae alipita kwa sharkter donestk kwa changamoto ya goli la ugenini lakini katika makundi alipita katika timu kama chelsea , Atletico Madrid na katika timu hizo kote alipata matokeo yaliyomsaidia kufika katika hatua hizi. Barcelona waliingia katika mchezo wakiwa na spirit ya kwamba mchezo umeisha toka nou camp ,walicheza kwa kujiamini kwamba hakuna maajabu yoyote yanaweza kutokea kwa vile tu walimchukulia kama mnyonge , huku wakiwa wamesahau kwamba hawajawahi kushinda katika stadio olimpio katika mechi 3 za mwisho a...

DUNIA YA SOCCER IMEJIFUNZA KITU.

Hamza matwany Usiku wa tarehe 10 &11-2018 ulikuwa moja ya siku ambazo timu kutoka SERIE A zimeonyesha kwamba mpira ni dakika 90 kwa mechi moja lakini ni 180 kwenye hatua ya mtoano hasa kwenye Champions league . Roma na juventus zilionekana timu ambazo mechi zao za marudiano zitakuwa rahisi kutokana na matokeo ambayo waliyapata mechi zao za kwanza Juve alipoteza mechi yake ya kwanza akiwa nyumbani kwa jumla ya goli 3-0 dhidi ya miamba ya jiji la madrid na Roma alifungwa 4-1 pale Nou camp. Mechi za marudio barcelona alimfuata Roma pale stadio olimpio na Roma alifanikiwa kupata ushindi wa goli 3-0 hivyo kufanya agg 4-4 na goli la ugenini lilimpa nafasi ya kusonga mbele. madrid alimkaribisha Juventus pale Stadio de bernabeu huku madrid wakimkosa naodha wake sergio ramos na Juventus wakimkosa paul dybala wote hao wakiwekwa nje kwa kadi. lakini juve aliusimamisha usiku kama Roma alivyofanya kwa kumfunga madrid goli 3-1 hivyo kufanya agg 4-3 , kitu ambacho hakikutazamwa na wengi kweny...