Skip to main content

TATHMINI KUELEKEA DAR DERBY AZAM VS YANGA SC.

Hamza matwany

Weekend hii kutakuwa na kati ya zile mechi kubwa kwenye vodacom premier league( vpl) kati ya wenyeji azam fc mabingwa wa afrika mashariki na kati ikikutana na mabingwa wa kihistoria wa ligi hyo yanga sc.

Ushindani wa yanga na azam unatenganishwa na goli moja na ushindi wa mechi moja kati yao

Yanga na azam zimekutana mara 18 kwenye vpl tangu zilipokutana kwa mara kwanza mwaka 2008 katika mechi hizo yanga amefanikiwa kushinda mechi 6 na azam ameshinda mara 5 huku wakitoka sare michezo 7.
Katika mechi hizo yanga amefunga magoli 26 na azam amefunga magoli 25.

Kwenye mashindano yote ambayo azam na yanga wamekutana takwimu zao ni kama ifuatavyo;
Wamekutana mara 31 yanga ameshinda mara 12 na azam ameshinda mara 11 huku wakiwa wametoka sare mara 8.
Huku yanga akiifunga magoli 41 na azam fc wakiwa wamefunga magoli 40.

UBORA WA VIKOSI VYAO KWA SASA

Kwa msimu huu azam amekuwa na matokeo mazuri katika vpl akiwa ajapoteza mchezo hata mmoja wa ligi na yupo nafasi ya pili katika msimamo wa ligi.
Azam ndio mabingwa wa mapinduzi cup mwaka 2018. Amekuwa na mwendelezo mzuri ukilinganisha na yanga msimu huu ambayo ikiwa ipo nafasi ya 3 ikiwa imepoteza mchezo 1 dhidi ya mbao.

Yanga kuelekea mchezo huo watawakosa wachezaji wake saba muhimu ; yohana mkomola, abdallah shaibu, amissi tambwe, kamusoko, ngoma,pato ngonyani pamoja na pius buswita kwa sababu wote wanaumwa, licha ya kuumwa buswita anatumikia adhabu yake ya kadi 3 za njano.

#TUKUTANE CHAMAZI COMPLEX

Comments

Popular posts from this blog

JEZI YA NYUMBANI YA BARCELONA MSIMU WA 2018/2019 IMEVUJA MTANDAONI

Hamza matwany Jezi ya barcelona ya msimu wa 18/19 ambayo inatengezwa na kampuni ya vifaa vya michezo vya nike imevuja mtandaoni. Jezi hiyo ambayo inafanana na jezi ambayo ilitumiwa na club hiyo mwaka 1998 miaka 20  nyuma imetengezwa katika namna hiyo ili kuenzi legends kwa klabu hiyo Jezi ya nyumbani itakuwa ina wekundu na mistari ya blue na bukta nyeusi pia socks zake ni nyeusi kama inavyoonekana kwenye hizo picha

UNYONGE WA ROMA ULIVYOWAPELEKA SEMI FINAL

Na Hamza matwany. Roma usiku wa tarehe 10/7/2018 ameweza kuushangaza ulimwengu kwa kile kitendo cha kumtoa fc Barcelona kwenye hatua ya robo fainali kwa kupindua matokeo ambapo mwanzoni alifungwa goli 4-1 nou camp na kufanikiw Kushinda goli 3-0 pale stadio olimpio jijini Roma. wapenzi wengi wa mchezo huu hawakumpa nafasi Roma kwenda hatua inayofuata katika michuano hii kwa sababu tu ndo timu pekee ilionekana kama dhaifu kwa timu zilizoingia hatua ya robo fainali. Roma ambae alipita kwa sharkter donestk kwa changamoto ya goli la ugenini lakini katika makundi alipita katika timu kama chelsea , Atletico Madrid na katika timu hizo kote alipata matokeo yaliyomsaidia kufika katika hatua hizi. Barcelona waliingia katika mchezo wakiwa na spirit ya kwamba mchezo umeisha toka nou camp ,walicheza kwa kujiamini kwamba hakuna maajabu yoyote yanaweza kutokea kwa vile tu walimchukulia kama mnyonge , huku wakiwa wamesahau kwamba hawajawahi kushinda katika stadio olimpio katika mechi 3 za mwisho a...

DUNIA YA SOCCER IMEJIFUNZA KITU.

Hamza matwany Usiku wa tarehe 10 &11-2018 ulikuwa moja ya siku ambazo timu kutoka SERIE A zimeonyesha kwamba mpira ni dakika 90 kwa mechi moja lakini ni 180 kwenye hatua ya mtoano hasa kwenye Champions league . Roma na juventus zilionekana timu ambazo mechi zao za marudiano zitakuwa rahisi kutokana na matokeo ambayo waliyapata mechi zao za kwanza Juve alipoteza mechi yake ya kwanza akiwa nyumbani kwa jumla ya goli 3-0 dhidi ya miamba ya jiji la madrid na Roma alifungwa 4-1 pale Nou camp. Mechi za marudio barcelona alimfuata Roma pale stadio olimpio na Roma alifanikiwa kupata ushindi wa goli 3-0 hivyo kufanya agg 4-4 na goli la ugenini lilimpa nafasi ya kusonga mbele. madrid alimkaribisha Juventus pale Stadio de bernabeu huku madrid wakimkosa naodha wake sergio ramos na Juventus wakimkosa paul dybala wote hao wakiwekwa nje kwa kadi. lakini juve aliusimamisha usiku kama Roma alivyofanya kwa kumfunga madrid goli 3-1 hivyo kufanya agg 4-3 , kitu ambacho hakikutazamwa na wengi kweny...