Skip to main content

FAHAMU MACHACHE KUHUSIANA NA EPL

Na Muller Idriss

Wakati michezo mbalimbali inaendelea kupigwa katika viwanja mbalimbali nchini Uingereza ikiwa ni muendelezo wa ligi kuu ya nchi hiyo maarufu kama EPL, Fahamu mambo kadha wa kadha kuhusiana na ligi hiyo:-
Manchester United ndiyo timu iliyotwaa ubingwa wa ligi hyo mara nyingi kuliko timu yoyote nchini humo.Imetwaa ubingwa wa ligi hiyo mara 13 tangu mwaka 1992.
Lakini pia Man united ndio timu timu iliyoweka rekodi ya kutwaa ubingwa huo  mara tatu mfululizo mnamo msimu wa mwaka 1998-99,199-2000 na 2000-2001 na waliifikia rekodi yao wenyewe mnamo mwaka 2006-07,2007-08 na 2008-09

Rekodi nyingine ni ya kutwaa ubingwa wa epl kwa tofauti ya pointi kubwa. Rekodi hiyo inashikiliwa na klabu ya Manchester United ambapo ilitwaa ubingwa huo kwa tofauti ya pointi 18 baada ya kufikisha pointi 91 wakifuatiwa na Arsenal ambao walifikisha pointi 73. Hiyo ikiwa ni tofauti kubwa ya pointi, tofauti ndogo kabisa ni tofauti ya pointi 0 ambayo iliwekwa mwaka 2011-12 ambapo Manchester city na Man united zilifikisha pointi 89 na ubingwa kuamuliwa kwa tofauti ya magoli, hivyo Man city aliibuka bingwa baada ya kuwa na tofauti ya magoli +64 na Man united +56 Hii ilikuwa ni mwaka wa kwanza kwa Ligi hii kuamuliwa kwa tofauti ya magoli.

Rekodi nyingine ni ya USHINDI.
Chelsea inashikilia rekodi ya kushinda michezo mingi kwa msimu ambapo wameshinda michezo 30 kati ya 38 waliyocheza mnamo 2016-17
Na Derby County ndiyo timu iliyoshinda michezo michache zaidi kwenye Ligi hiyo ambapo ilishinda mchezo mmoja (1)tu kati ya 38 waliyocheza mnamo mwaka 2007-08.

Kwa hayo na mengine mengi endelea kutufatilia katika mitandao ya kijamii
Instagram

Chillu_soccer
Muller Idriss

Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

JEZI YA NYUMBANI YA BARCELONA MSIMU WA 2018/2019 IMEVUJA MTANDAONI

Hamza matwany Jezi ya barcelona ya msimu wa 18/19 ambayo inatengezwa na kampuni ya vifaa vya michezo vya nike imevuja mtandaoni. Jezi hiyo ambayo inafanana na jezi ambayo ilitumiwa na club hiyo mwaka 1998 miaka 20  nyuma imetengezwa katika namna hiyo ili kuenzi legends kwa klabu hiyo Jezi ya nyumbani itakuwa ina wekundu na mistari ya blue na bukta nyeusi pia socks zake ni nyeusi kama inavyoonekana kwenye hizo picha

UNYONGE WA ROMA ULIVYOWAPELEKA SEMI FINAL

Na Hamza matwany. Roma usiku wa tarehe 10/7/2018 ameweza kuushangaza ulimwengu kwa kile kitendo cha kumtoa fc Barcelona kwenye hatua ya robo fainali kwa kupindua matokeo ambapo mwanzoni alifungwa goli 4-1 nou camp na kufanikiw Kushinda goli 3-0 pale stadio olimpio jijini Roma. wapenzi wengi wa mchezo huu hawakumpa nafasi Roma kwenda hatua inayofuata katika michuano hii kwa sababu tu ndo timu pekee ilionekana kama dhaifu kwa timu zilizoingia hatua ya robo fainali. Roma ambae alipita kwa sharkter donestk kwa changamoto ya goli la ugenini lakini katika makundi alipita katika timu kama chelsea , Atletico Madrid na katika timu hizo kote alipata matokeo yaliyomsaidia kufika katika hatua hizi. Barcelona waliingia katika mchezo wakiwa na spirit ya kwamba mchezo umeisha toka nou camp ,walicheza kwa kujiamini kwamba hakuna maajabu yoyote yanaweza kutokea kwa vile tu walimchukulia kama mnyonge , huku wakiwa wamesahau kwamba hawajawahi kushinda katika stadio olimpio katika mechi 3 za mwisho a...

DUNIA YA SOCCER IMEJIFUNZA KITU.

Hamza matwany Usiku wa tarehe 10 &11-2018 ulikuwa moja ya siku ambazo timu kutoka SERIE A zimeonyesha kwamba mpira ni dakika 90 kwa mechi moja lakini ni 180 kwenye hatua ya mtoano hasa kwenye Champions league . Roma na juventus zilionekana timu ambazo mechi zao za marudiano zitakuwa rahisi kutokana na matokeo ambayo waliyapata mechi zao za kwanza Juve alipoteza mechi yake ya kwanza akiwa nyumbani kwa jumla ya goli 3-0 dhidi ya miamba ya jiji la madrid na Roma alifungwa 4-1 pale Nou camp. Mechi za marudio barcelona alimfuata Roma pale stadio olimpio na Roma alifanikiwa kupata ushindi wa goli 3-0 hivyo kufanya agg 4-4 na goli la ugenini lilimpa nafasi ya kusonga mbele. madrid alimkaribisha Juventus pale Stadio de bernabeu huku madrid wakimkosa naodha wake sergio ramos na Juventus wakimkosa paul dybala wote hao wakiwekwa nje kwa kadi. lakini juve aliusimamisha usiku kama Roma alivyofanya kwa kumfunga madrid goli 3-1 hivyo kufanya agg 4-3 , kitu ambacho hakikutazamwa na wengi kweny...