Skip to main content

NAMFAHAMU VIZURI ABRAMOVICH CONTE JIANDAE

Hamza matwani
chelsea ni moja ya club duniani zinazomilikiwa na mtu binafsi ambae ni Roman abramovich , lakini boss huyo anatambulika kwa kutoweza kumvulia kocha ikiwa timu inapata matokeo mabaya japo kwa msimu mmoja :

Antonio conte anakuwa kocha wa 16 kuifundisha chelsea toka mwaka 2000 kwa wastani kila kocha amedumu kwenye club hiyo kwa mwaka mmoja na mwezi mmoja. :

makocha mashughuli duniani wamepita kwenye club hiyo tangu mwaka 2000 mfano josë mourinho, fellipe scolari, claudio ranieri, Rafa benitez, Guus huddink, Andre villa boas, carlo anceloti, steve holland, ray wilkins , Roberto di mateo na wengine wengi. :  Antonio conte mkataba wake unamalizika mwaka 2021 lakini sitarajii kuona akimaliza mkataba huo kwa muda husika bila kutupiwa vilago vyako. :

unamkumbuka Roberto di mateo kocha pekee aliewapa taji la UEFA club hiyo kwa kupita katika migongo ya timu ngumu duniani akifanya come back ya historia pale darajani kwa kuwafunga napoli jumla ya goli 4-1baada ya kufungwa kwenye first leg na Napoli goli 3 -1.Baadae alifanikiwa kumfunga barcelona na kucheza fainali na Bayern na kupata ubingwa ambao ni historia kwa club. Lakini baada ya mwaka mmoja tu alitimuliwa kwenye club hiyo. :
mpaka sasa sioni sababu ya kusema conte atabaki mpaka mwaka 2021 ikiwa timu inapigania kucheza UEROPA msimu ujao, akitoka kuwa bingwa msimu uliopita , huku akipata matokeo mabaya kwenye mechi za hivi karibuni. :

Amepoteza mchezo dhidi ya barca, katoka kupoteza dhidi ya totnham, na jana tu akitoka kutoa sare na westham nyumbani. :

Sitashangaa kumuona manager mpya akiwa na chelsea msimu ujao kwa sababu tu namfahamu Roman abramovich.

Comments

Popular posts from this blog

JEZI YA NYUMBANI YA BARCELONA MSIMU WA 2018/2019 IMEVUJA MTANDAONI

Hamza matwany Jezi ya barcelona ya msimu wa 18/19 ambayo inatengezwa na kampuni ya vifaa vya michezo vya nike imevuja mtandaoni. Jezi hiyo ambayo inafanana na jezi ambayo ilitumiwa na club hiyo mwaka 1998 miaka 20  nyuma imetengezwa katika namna hiyo ili kuenzi legends kwa klabu hiyo Jezi ya nyumbani itakuwa ina wekundu na mistari ya blue na bukta nyeusi pia socks zake ni nyeusi kama inavyoonekana kwenye hizo picha

UNYONGE WA ROMA ULIVYOWAPELEKA SEMI FINAL

Na Hamza matwany. Roma usiku wa tarehe 10/7/2018 ameweza kuushangaza ulimwengu kwa kile kitendo cha kumtoa fc Barcelona kwenye hatua ya robo fainali kwa kupindua matokeo ambapo mwanzoni alifungwa goli 4-1 nou camp na kufanikiw Kushinda goli 3-0 pale stadio olimpio jijini Roma. wapenzi wengi wa mchezo huu hawakumpa nafasi Roma kwenda hatua inayofuata katika michuano hii kwa sababu tu ndo timu pekee ilionekana kama dhaifu kwa timu zilizoingia hatua ya robo fainali. Roma ambae alipita kwa sharkter donestk kwa changamoto ya goli la ugenini lakini katika makundi alipita katika timu kama chelsea , Atletico Madrid na katika timu hizo kote alipata matokeo yaliyomsaidia kufika katika hatua hizi. Barcelona waliingia katika mchezo wakiwa na spirit ya kwamba mchezo umeisha toka nou camp ,walicheza kwa kujiamini kwamba hakuna maajabu yoyote yanaweza kutokea kwa vile tu walimchukulia kama mnyonge , huku wakiwa wamesahau kwamba hawajawahi kushinda katika stadio olimpio katika mechi 3 za mwisho a...

DUNIA YA SOCCER IMEJIFUNZA KITU.

Hamza matwany Usiku wa tarehe 10 &11-2018 ulikuwa moja ya siku ambazo timu kutoka SERIE A zimeonyesha kwamba mpira ni dakika 90 kwa mechi moja lakini ni 180 kwenye hatua ya mtoano hasa kwenye Champions league . Roma na juventus zilionekana timu ambazo mechi zao za marudiano zitakuwa rahisi kutokana na matokeo ambayo waliyapata mechi zao za kwanza Juve alipoteza mechi yake ya kwanza akiwa nyumbani kwa jumla ya goli 3-0 dhidi ya miamba ya jiji la madrid na Roma alifungwa 4-1 pale Nou camp. Mechi za marudio barcelona alimfuata Roma pale stadio olimpio na Roma alifanikiwa kupata ushindi wa goli 3-0 hivyo kufanya agg 4-4 na goli la ugenini lilimpa nafasi ya kusonga mbele. madrid alimkaribisha Juventus pale Stadio de bernabeu huku madrid wakimkosa naodha wake sergio ramos na Juventus wakimkosa paul dybala wote hao wakiwekwa nje kwa kadi. lakini juve aliusimamisha usiku kama Roma alivyofanya kwa kumfunga madrid goli 3-1 hivyo kufanya agg 4-3 , kitu ambacho hakikutazamwa na wengi kweny...