Skip to main content

KUELEKEA MCHEZO KATI YA PSG NA REAL MADRID

  Na Muller Idriss
Mnamo tar 11 Dec droo ya michuano ya klabu bingwa barani ulaya maarufu kama Uefa ilifanyika na moja kati ya mchezo ulioamsha hisia za wengi hususani wadau wa mchezo wa soka ni mchezo kati ya wababe wa ufaransa PSG dhidi ya Real Madrid.
Japo wengi wanautazama mchezo huu kwa kumpa PSG nafasi kubwa ya kushinda na wachache wakimpa Real Madrid kwa sababu ya historia yake kwenye michuano hii ya uefa.

Real madrid ndio mabingwa mara kumi na mbili katika michuano hii huku PSG wakiwa hawajawahi kupata ubingwa wa michuano  hii tangu kuanzishwa kwake.
   Hizi timu zimekutana mara 7 tangu kuanzishwa kwa hizi timu huku mara sita (6) kati ya hizo ikiwa ni michuano mbalimbali barani ulaya na mara moja ikiwa ni mechi ya kirafiki (pre_season)
Kwa mara ya kwanza timu hizi zilikutana msimu wa mwaka 1992/93 ambapo mchezo wa kwanza Madrid alishinda nyumbani kwa mabao 3_1 na waliporudi Ufaransa, wababe hao wa Hispania walikubali kupokea kichapo cha mabao 4_1 hivyo Real Madrid kuondolewa kwenye michuano hiyo.
   Mara ya tatu ni msimu wa mwaka 1994/1995 ambapo mchezo wa kwanza Real Madrid akiwa nyumbani alikubali kichapo cha bao moja kwa bila 1_0 kutoka kwa PSG na waliporudi Ufaransa mchezo ulimalizika kwa sare ya bila kufungana na kukamilisha jumla ya michezo minne.
    Mwaka 2015 timu hizo zilikutana katika michuano hii zikiwa zimepangwa kundi moja ambapo mchezo wa kwanza ulimalizika   kwa sare ya bila kufungana pale Ufaransa na waliporudi Hispania PSG walikubali kipigo cha bao moja kwa bila (1_0).
Na mara ya mwisho walikutana katika pre season mwaka 2016 na Real madrid ililazwa bao 3 kwa 1
Kwa ujumla wake PSG ameshinda michezo mitatu kati ya 7 waliyokutana na Real madrid akishinda michezo 2 kati ya hiyo 7 na wakitoka sare mara 2.
Ukiachana na Historia hizo tuje kuangalia perfomance ya timu hizi mbili kwa sasa..PSG wapo juu kwenye msimamo wa ligi huku Real madrid wakiwa katika nafasi ya tatu kwenye La liga. Safu ya ushambuliaji ya PSG ikiwajumlisha Neymar,Mbappe na Cavanni imefunga magoli 32 mpaka sasa kwenye league 1 huku ile ya Real Madrid Ronaldo,Isco na Asensio ikiwa imefunga magoli 12 tu kwenye La liga pia safu ya PSG imefunga magoli 16 kwenye Uefa mpka sas na madrid ikiwa imefunga magoli 12
Kwa upande wangu nautazama mchezo huu kama mchezo mmoja mzuri sana ambao dunia itashuhudia historia nyingine ikiwekwa katika soka barani ulaya

Comments

Popular posts from this blog

JEZI YA NYUMBANI YA BARCELONA MSIMU WA 2018/2019 IMEVUJA MTANDAONI

Hamza matwany Jezi ya barcelona ya msimu wa 18/19 ambayo inatengezwa na kampuni ya vifaa vya michezo vya nike imevuja mtandaoni. Jezi hiyo ambayo inafanana na jezi ambayo ilitumiwa na club hiyo mwaka 1998 miaka 20  nyuma imetengezwa katika namna hiyo ili kuenzi legends kwa klabu hiyo Jezi ya nyumbani itakuwa ina wekundu na mistari ya blue na bukta nyeusi pia socks zake ni nyeusi kama inavyoonekana kwenye hizo picha

KOCHA WA STARS ATANGAZA KIKOSI CHA COSAFA

Kocha Mkuu wa timu ya Tanzania ‘Taifa Stars’, Salum Shabani Mayanga,  Jumatano Juni 14, 2017 ametangaza majina ya wachezaji 22 watakaounda kikosi kinachokwenda kushindana kuwania Kombe la Castle Cosafa nchini Afrika Kusini. Taifa Stars inayodhaminiwa na Bia ya Serengeti, inatarajiwa kuanza kambi rasmi kesho Jumapili Juni 18, mwaka huu. Kambi hiyo itakuwa kwenye Hoteli ya Urban Rose, iliyoko Mtaa wa Jamhuri katikati ya jiji la Dar es Salaam. Taifa Stars inajiandaa na michuano ya Cosafa inayotarajiwa kuanza Juni 25, mwaka huu. Michuano hiyo, inaandaliwa na Baraza la Mpira wa Miguu la nchi za Kusini mwa Afrika ambako Tanzania – mwanachama wa Cecafa, imepata mwaliko kushiriki. Tanzania imepangwa kundi A ambako wapinzani wake ni Mauritius, Malawi na Angola wakati Kundi B ni Msumbiji, Shelisheli, Madagascar na Zimbabwe. Timu za Botswana, Zambia na Afrika Kusini kadhalika Namibia, Lesotho na Swaziland zitakuwa na mechi maalumu (play off) ili kuingia robo fainali. Kwa mujibu wa Mayanga...

DEMBELE OUT WIKI 4

Hamza matwany Madaktari wa klabu ya barcelona wamethibitisha osmanè dembele raia wa ufaransa atakuwa nje kwa wiki 3 hadi 4 kutokana na majeraha ya msuli ambayo aliyapata kwenye mechi dhidi ya real socieded kwenye uwanja wa anoeta jumapili Mchezaji huyo akiwa ametoka kwenye majeraha ya muda mrefu baada ya kukaa nje kwa miezi minne tangu alipoumia mwezi wa nane kwenye mechi dhidi ya getafe. Madaktari wa klabu wamethibitisha majeraha hayo hayata athiri lile jeraha lake la kwanza la upasuaji alilofanya mwezi wa 8 Bado osmane dembele ajakuwa na wakati mzuri kutokana na majehara hayo yanamsumbua.