Skip to main content

NINI KIMEMPONZA YANGA MBELE YA MBAO?

Na Hamza matwany

Katika mchezo ambao umepigwa katika uwanja wa ccm kirumba mnamo tarehe 31/12/2017 umezikutanisha timu ambazo zinazidi kuwa na upinzani mkubwa kadri miaka inavyozidi kwenda ni mbao fc vs yanga sc.

Katika michezo mitatu mfululizo yanga anapoteza mechi katika uwanja wa ccm kirumba. Hivyo mbao kujivunia historia pekee dhidi ya yanga katika uwanja wake wa nyumbani.

Ni nini kimeiponza yanga katika mchezo huo? Moja wa sababu ni kuwakosa wachezaji wake muhimu akiwemo obrey chirwa, ibrahimu migomba ajibu, thaban kamusoko na wengine wengi ambao wamekuwa msaada kwa klabu ya yanga ndani ya mwaka huu.

Pia yanga imecheza na timu yenye upinzani mkubwa kwao bila ya kuwa na kocha wao mkuu ambae amepata matatizo ya kifamilia, kwa hiyo timu iliongozwa na kocha msaidizi pengine mbinu za kiufundi zilimshinda katika mchezo huo wa jana.

Team chemistry pia ilikosekana kwa wachezaji ambao walicheza katika kikosi hicho kwa mfano abdallah shaibu alipata nafasi ya kuanza katika kikosi cha kwanza kwa mara ya kwanza kwenye ligi kuu tangu asajilie kwa hiyo hapakuwa na chemistry mzuri kati yake na andrew vicent hivyo walimfanya Habibu kiyombo kuwa shujaa katika eneo hilo na mchezo wote kwa ujumla.

Pia katika nafasi ya ushambuliaji Amis tambwe aliongoza mashambulizi ya yanga huku akiwa ndo mchezo wake wa kwanza wa ligi kuu tangu arudi katika majeraha yake, hivyo hakuweza kuleta usumbufu mkubwa na ilikuwa kazi rahisi kwa ulinzi wa mbao kumzuia ikiongozwa na yusuf ndikumana.

Pia katika nafasi ya mashabiki mbao huwa wanakuwa na advantage kubwa ya mashabiki wenye morali kwenye michezo yao dhidi ya timu kubwa zinapofika ccm kirumba.

Comments

Popular posts from this blog

JEZI YA NYUMBANI YA BARCELONA MSIMU WA 2018/2019 IMEVUJA MTANDAONI

Hamza matwany Jezi ya barcelona ya msimu wa 18/19 ambayo inatengezwa na kampuni ya vifaa vya michezo vya nike imevuja mtandaoni. Jezi hiyo ambayo inafanana na jezi ambayo ilitumiwa na club hiyo mwaka 1998 miaka 20  nyuma imetengezwa katika namna hiyo ili kuenzi legends kwa klabu hiyo Jezi ya nyumbani itakuwa ina wekundu na mistari ya blue na bukta nyeusi pia socks zake ni nyeusi kama inavyoonekana kwenye hizo picha

KOCHA WA STARS ATANGAZA KIKOSI CHA COSAFA

Kocha Mkuu wa timu ya Tanzania ‘Taifa Stars’, Salum Shabani Mayanga,  Jumatano Juni 14, 2017 ametangaza majina ya wachezaji 22 watakaounda kikosi kinachokwenda kushindana kuwania Kombe la Castle Cosafa nchini Afrika Kusini. Taifa Stars inayodhaminiwa na Bia ya Serengeti, inatarajiwa kuanza kambi rasmi kesho Jumapili Juni 18, mwaka huu. Kambi hiyo itakuwa kwenye Hoteli ya Urban Rose, iliyoko Mtaa wa Jamhuri katikati ya jiji la Dar es Salaam. Taifa Stars inajiandaa na michuano ya Cosafa inayotarajiwa kuanza Juni 25, mwaka huu. Michuano hiyo, inaandaliwa na Baraza la Mpira wa Miguu la nchi za Kusini mwa Afrika ambako Tanzania – mwanachama wa Cecafa, imepata mwaliko kushiriki. Tanzania imepangwa kundi A ambako wapinzani wake ni Mauritius, Malawi na Angola wakati Kundi B ni Msumbiji, Shelisheli, Madagascar na Zimbabwe. Timu za Botswana, Zambia na Afrika Kusini kadhalika Namibia, Lesotho na Swaziland zitakuwa na mechi maalumu (play off) ili kuingia robo fainali. Kwa mujibu wa Mayanga...

DEMBELE OUT WIKI 4

Hamza matwany Madaktari wa klabu ya barcelona wamethibitisha osmanè dembele raia wa ufaransa atakuwa nje kwa wiki 3 hadi 4 kutokana na majeraha ya msuli ambayo aliyapata kwenye mechi dhidi ya real socieded kwenye uwanja wa anoeta jumapili Mchezaji huyo akiwa ametoka kwenye majeraha ya muda mrefu baada ya kukaa nje kwa miezi minne tangu alipoumia mwezi wa nane kwenye mechi dhidi ya getafe. Madaktari wa klabu wamethibitisha majeraha hayo hayata athiri lile jeraha lake la kwanza la upasuaji alilofanya mwezi wa 8 Bado osmane dembele ajakuwa na wakati mzuri kutokana na majehara hayo yanamsumbua.