Skip to main content

MAJERAHA MAKUBWA LIGI 5 KUBWA BARANI ULAYA

Hamza matwany
Hivi unawajua wachezaji waliowahi kupata majeraha makubwa na kukaa nje siku nyingi pia kukosa michezo mingi kwenye vilabu vyao?

Nmekuletea hizi takwimu za wachezaji wa ligi kubwa 5 barani ulaya kwa idadi ya majeraha waliyoyapata, siku walizokaa mpaka kupona hayo majeraha yote na michezo pia ambayo wameikosa.

Premier league( EPL)
Kwa upande wa ligi kuu kijana mwenye kipaji kikubwa raia wa uingereza na klabu ya arsenal Jack wilshere ndio anaongoza kwenye ligi hii akiwa amepata majeraha mara 13 akiwa ametumia siku 1013 kuuguza majeraha hayo yote .Jack wilshere amekosa michezo 155 mpaka sasa kipindi chote alichoapata majeraha hayo.

La liga (santander)
Kwenye ligi hii Thomas vermalein mchezaji wa fc barcelona pamoja na taifa ya ubelgiji ndio anaeongoza kwa majeraha mengi kwenye ligi hii akiwa ameumia mara 23 akiwa ametumia siku 1026 katika kuuguza majeraha yote ambayo ameyapata akiwa amekosa michezo 128 katika kipind chote cha majeraha.

Bundersliga
Kwenye ligi kuu ujerumani marco reus wa klabu ya dortmund na taifa la ujerumani ndio anaongoza kwa majeraha mengi zaidi akiwa ameumia mara 41 akiwa ametumia siku 813 kuuguza yote hayo ,huku akiwa amekosa michezo 104 akiwa katika kipindi hicho kigumu.

Seria A
Giuseppe rossi raia wa italy na klabu ya genoa ndio anaongoza kwenye ligi hii akiwa ameumia mara 7 akitumia siku 1194 kuuguza mjeraha hayo huku akiwa amekosa michezo 148 katika kipindi hicho chote.

Ligue 1
Katika ligi kuu nchini ufaransa mchezaji wa marseille na taifa la ufaransa Abou diaby ndio anaongoza akiwa ameumia mara 21 akitumia siku 2072 kuuguza majeraha hayo yote akiwa amekosa mechi 368 katika kipindi chote cha maisha yake ya soka.
Pengine ndio akawa mchezaji wa kwanza mwenye majeraha hatari ya soka kwenye ligi hizi

Comments

Popular posts from this blog

JEZI YA NYUMBANI YA BARCELONA MSIMU WA 2018/2019 IMEVUJA MTANDAONI

Hamza matwany Jezi ya barcelona ya msimu wa 18/19 ambayo inatengezwa na kampuni ya vifaa vya michezo vya nike imevuja mtandaoni. Jezi hiyo ambayo inafanana na jezi ambayo ilitumiwa na club hiyo mwaka 1998 miaka 20  nyuma imetengezwa katika namna hiyo ili kuenzi legends kwa klabu hiyo Jezi ya nyumbani itakuwa ina wekundu na mistari ya blue na bukta nyeusi pia socks zake ni nyeusi kama inavyoonekana kwenye hizo picha

KOCHA WA STARS ATANGAZA KIKOSI CHA COSAFA

Kocha Mkuu wa timu ya Tanzania ‘Taifa Stars’, Salum Shabani Mayanga,  Jumatano Juni 14, 2017 ametangaza majina ya wachezaji 22 watakaounda kikosi kinachokwenda kushindana kuwania Kombe la Castle Cosafa nchini Afrika Kusini. Taifa Stars inayodhaminiwa na Bia ya Serengeti, inatarajiwa kuanza kambi rasmi kesho Jumapili Juni 18, mwaka huu. Kambi hiyo itakuwa kwenye Hoteli ya Urban Rose, iliyoko Mtaa wa Jamhuri katikati ya jiji la Dar es Salaam. Taifa Stars inajiandaa na michuano ya Cosafa inayotarajiwa kuanza Juni 25, mwaka huu. Michuano hiyo, inaandaliwa na Baraza la Mpira wa Miguu la nchi za Kusini mwa Afrika ambako Tanzania – mwanachama wa Cecafa, imepata mwaliko kushiriki. Tanzania imepangwa kundi A ambako wapinzani wake ni Mauritius, Malawi na Angola wakati Kundi B ni Msumbiji, Shelisheli, Madagascar na Zimbabwe. Timu za Botswana, Zambia na Afrika Kusini kadhalika Namibia, Lesotho na Swaziland zitakuwa na mechi maalumu (play off) ili kuingia robo fainali. Kwa mujibu wa Mayanga...

DEMBELE OUT WIKI 4

Hamza matwany Madaktari wa klabu ya barcelona wamethibitisha osmanè dembele raia wa ufaransa atakuwa nje kwa wiki 3 hadi 4 kutokana na majeraha ya msuli ambayo aliyapata kwenye mechi dhidi ya real socieded kwenye uwanja wa anoeta jumapili Mchezaji huyo akiwa ametoka kwenye majeraha ya muda mrefu baada ya kukaa nje kwa miezi minne tangu alipoumia mwezi wa nane kwenye mechi dhidi ya getafe. Madaktari wa klabu wamethibitisha majeraha hayo hayata athiri lile jeraha lake la kwanza la upasuaji alilofanya mwezi wa 8 Bado osmane dembele ajakuwa na wakati mzuri kutokana na majehara hayo yanamsumbua.