Skip to main content

FAHAMU MACHACHE KUHUSIANA NA EPL

Na Muller Idriss

Wakati michezo mbalimbali inaendelea kupigwa katika viwanja mbalimbali nchini Uingereza ikiwa ni muendelezo wa ligi kuu ya nchi hiyo maarufu kama EPL, Fahamu mambo kadha wa kadha kuhusiana na ligi hiyo:-
Manchester United ndiyo timu iliyotwaa ubingwa wa ligi hyo mara nyingi kuliko timu yoyote nchini humo.Imetwaa ubingwa wa ligi hiyo mara 13 tangu mwaka 1992.
Lakini pia Man united ndio timu timu iliyoweka rekodi ya kutwaa ubingwa huo  mara tatu mfululizo mnamo msimu wa mwaka 1998-99,199-2000 na 2000-2001 na waliifikia rekodi yao wenyewe mnamo mwaka 2006-07,2007-08 na 2008-09

Rekodi nyingine ni ya kutwaa ubingwa wa epl kwa tofauti ya pointi kubwa. Rekodi hiyo inashikiliwa na klabu ya Manchester United ambapo ilitwaa ubingwa huo kwa tofauti ya pointi 18 baada ya kufikisha pointi 91 wakifuatiwa na Arsenal ambao walifikisha pointi 73. Hiyo ikiwa ni tofauti kubwa ya pointi, tofauti ndogo kabisa ni tofauti ya pointi 0 ambayo iliwekwa mwaka 2011-12 ambapo Manchester city na Man united zilifikisha pointi 89 na ubingwa kuamuliwa kwa tofauti ya magoli, hivyo Man city aliibuka bingwa baada ya kuwa na tofauti ya magoli +64 na Man united +56 Hii ilikuwa ni mwaka wa kwanza kwa Ligi hii kuamuliwa kwa tofauti ya magoli.

Rekodi nyingine ni ya USHINDI.
Chelsea inashikilia rekodi ya kushinda michezo mingi kwa msimu ambapo wameshinda michezo 30 kati ya 38 waliyocheza mnamo 2016-17
Na Derby County ndiyo timu iliyoshinda michezo michache zaidi kwenye Ligi hiyo ambapo ilishinda mchezo mmoja (1)tu kati ya 38 waliyocheza mnamo mwaka 2007-08.

Kwa hayo na mengine mengi endelea kutufatilia katika mitandao ya kijamii
Instagram

Chillu_soccer
Muller Idriss

Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

JEZI YA NYUMBANI YA BARCELONA MSIMU WA 2018/2019 IMEVUJA MTANDAONI

Hamza matwany Jezi ya barcelona ya msimu wa 18/19 ambayo inatengezwa na kampuni ya vifaa vya michezo vya nike imevuja mtandaoni. Jezi hiyo ambayo inafanana na jezi ambayo ilitumiwa na club hiyo mwaka 1998 miaka 20  nyuma imetengezwa katika namna hiyo ili kuenzi legends kwa klabu hiyo Jezi ya nyumbani itakuwa ina wekundu na mistari ya blue na bukta nyeusi pia socks zake ni nyeusi kama inavyoonekana kwenye hizo picha

KOCHA WA STARS ATANGAZA KIKOSI CHA COSAFA

Kocha Mkuu wa timu ya Tanzania ‘Taifa Stars’, Salum Shabani Mayanga,  Jumatano Juni 14, 2017 ametangaza majina ya wachezaji 22 watakaounda kikosi kinachokwenda kushindana kuwania Kombe la Castle Cosafa nchini Afrika Kusini. Taifa Stars inayodhaminiwa na Bia ya Serengeti, inatarajiwa kuanza kambi rasmi kesho Jumapili Juni 18, mwaka huu. Kambi hiyo itakuwa kwenye Hoteli ya Urban Rose, iliyoko Mtaa wa Jamhuri katikati ya jiji la Dar es Salaam. Taifa Stars inajiandaa na michuano ya Cosafa inayotarajiwa kuanza Juni 25, mwaka huu. Michuano hiyo, inaandaliwa na Baraza la Mpira wa Miguu la nchi za Kusini mwa Afrika ambako Tanzania – mwanachama wa Cecafa, imepata mwaliko kushiriki. Tanzania imepangwa kundi A ambako wapinzani wake ni Mauritius, Malawi na Angola wakati Kundi B ni Msumbiji, Shelisheli, Madagascar na Zimbabwe. Timu za Botswana, Zambia na Afrika Kusini kadhalika Namibia, Lesotho na Swaziland zitakuwa na mechi maalumu (play off) ili kuingia robo fainali. Kwa mujibu wa Mayanga...

DEMBELE OUT WIKI 4

Hamza matwany Madaktari wa klabu ya barcelona wamethibitisha osmanè dembele raia wa ufaransa atakuwa nje kwa wiki 3 hadi 4 kutokana na majeraha ya msuli ambayo aliyapata kwenye mechi dhidi ya real socieded kwenye uwanja wa anoeta jumapili Mchezaji huyo akiwa ametoka kwenye majeraha ya muda mrefu baada ya kukaa nje kwa miezi minne tangu alipoumia mwezi wa nane kwenye mechi dhidi ya getafe. Madaktari wa klabu wamethibitisha majeraha hayo hayata athiri lile jeraha lake la kwanza la upasuaji alilofanya mwezi wa 8 Bado osmane dembele ajakuwa na wakati mzuri kutokana na majehara hayo yanamsumbua.