Skip to main content

ARDA TURAN NA MAISHA MAPYA YA SOCCER

Hamza matwany
Klabu ya barcelona rasmi imemuachia mchezaji wake arda turan kwa mkopo kwenye klabu ya kséhīr ya nchini uturuki.

Arda turan  30 atakuwa kwa mkopo wa miaka 2 na nusu  katika klabu hiyo na baada ya hapo barcelona wanaweza kumuuza kwenye klabu yoyote ya ulaya na pia kwenye mkataba wake wa mkopo kuna kipengele cha mkopo ambacho kinawaruhusu instabul basaksehir kumnunua kwa jumla baada ya muda huo wa mkopo  na rasmi jana ametambulishwa kwenye klabu hiyo ya uturuki.

Barca walimnunua arda turan kutoka atletico madrid akiwa kwenye kiwango kizuri sana lakini mambo hayakumuendea sawa akiwa na fc barcelona

Arda turan aliandamwa na majeruhi ya muda mrefu katika club hiyo hali iliyomfanya akose nafasi ya kucheza katika klabu hiyo.

Arda turan amedumu  katika ligi kuu spain kwa misimu sita na ameshinda la liga, europa league .

Alijiunga na atletico madrid akitokea klabu ya galatasaray ya nchini kwao uturuki, pia likiwa zao ya galatasaray youth academy.

Comments

Popular posts from this blog

USAJILI MPYA EVERTON

Baada ya kukamilisha usajili wa golikipa pickford . Everton wamekamilisha usajili wa kiungo toka club ya Fc ajax ya holland davy klaassen kwa uhamisho wa €27m Ambae alioongoza club hyo mpaka fainali ya ueropa league msimu uliomalizika kabla kufungwa na manchester united Yeye akiwa kama captain ya club hyo

KOCHA WA STARS ATANGAZA KIKOSI CHA COSAFA

Kocha Mkuu wa timu ya Tanzania ‘Taifa Stars’, Salum Shabani Mayanga,  Jumatano Juni 14, 2017 ametangaza majina ya wachezaji 22 watakaounda kikosi kinachokwenda kushindana kuwania Kombe la Castle Cosafa nchini Afrika Kusini. Taifa Stars inayodhaminiwa na Bia ya Serengeti, inatarajiwa kuanza kambi rasmi kesho Jumapili Juni 18, mwaka huu. Kambi hiyo itakuwa kwenye Hoteli ya Urban Rose, iliyoko Mtaa wa Jamhuri katikati ya jiji la Dar es Salaam. Taifa Stars inajiandaa na michuano ya Cosafa inayotarajiwa kuanza Juni 25, mwaka huu. Michuano hiyo, inaandaliwa na Baraza la Mpira wa Miguu la nchi za Kusini mwa Afrika ambako Tanzania – mwanachama wa Cecafa, imepata mwaliko kushiriki. Tanzania imepangwa kundi A ambako wapinzani wake ni Mauritius, Malawi na Angola wakati Kundi B ni Msumbiji, Shelisheli, Madagascar na Zimbabwe. Timu za Botswana, Zambia na Afrika Kusini kadhalika Namibia, Lesotho na Swaziland zitakuwa na mechi maalumu (play off) ili kuingia robo fainali. Kwa mujibu wa Mayanga...

JEZI YA NYUMBANI YA BARCELONA MSIMU WA 2018/2019 IMEVUJA MTANDAONI

Hamza matwany Jezi ya barcelona ya msimu wa 18/19 ambayo inatengezwa na kampuni ya vifaa vya michezo vya nike imevuja mtandaoni. Jezi hiyo ambayo inafanana na jezi ambayo ilitumiwa na club hiyo mwaka 1998 miaka 20  nyuma imetengezwa katika namna hiyo ili kuenzi legends kwa klabu hiyo Jezi ya nyumbani itakuwa ina wekundu na mistari ya blue na bukta nyeusi pia socks zake ni nyeusi kama inavyoonekana kwenye hizo picha