Skip to main content

MACHACHE KUELEKEA MCHEZO WA REAL SOCIEDED DHIDI YA BARCELONA

Hamza matwany
Kuelekea mchezo wa real socieded dhidi ya barcelona leo katika uwanja wa nyumbani wa real socieded Anoeta stadium, hizi ni takwimu chache kabla ya mchezo huo

Barcelona wanaongoza ligi kwa point 48 huku real socieded wakiwa nafasi ya 13 kwa point 23 katika michezo 18.

Kwenye mechi 7 za mwisho za la liga katika uwanja wa anoeta barcelona hawajawahi kushinda mchezo hata mmoja kati ya hiyo wamefungwa michezo 5 na kutoa sare mara mbili.

Mara ya mwisho barcelona kumfunga real socieded katika uwanja wake wa nyumbani ilikuwa mwaka 2007 katika ushindi wa goli 2_0

Mpaka sasa kwenye mechi 6 za mwisho za ligi real socieded ajashinda mchezo wowote amefungwa michezo 3 na kutoa sare michezo 3 msimu huu

Barcelona hajaruhusu goli lolote katika mechi zake 4 za mwisho za laliga msimu huu mara ya mwisho kufanya hivyo ilikuwa may 2016.

Real socieded  wamefunga magoli 6 katika dakika 15 za mwanzo kwenye la liga msimu huu.

Messi ndo kinara wa magoli kwenye mechi hii akiwa amefunga magoli 14 kati ya michezo 19 aliyocheza dhidi ya real socieded katika mashindano yote. Na kati ya hayo yote magoli 4 tu ndio kafunga kwenye uwanja wa anoeta.

Jordi alba na sergio roberto ndio wachezaji wanaoongoza kumpa assist mchezaji mmoja kila mmoja akifanya hivyo mara 5
Jordi alba vs messi
Sergio roberto vs suarez.

Ernesto valvede kocha wa barcelona ameshinda mara 5 katoa sare mara 6 kafungwa mara 4 katika awamu zote 15 ambazo amecheza dhidi ya real socieded.

LEO NINI KITATOKEA?

Comments

Popular posts from this blog

USAJILI MPYA EVERTON

Baada ya kukamilisha usajili wa golikipa pickford . Everton wamekamilisha usajili wa kiungo toka club ya Fc ajax ya holland davy klaassen kwa uhamisho wa €27m Ambae alioongoza club hyo mpaka fainali ya ueropa league msimu uliomalizika kabla kufungwa na manchester united Yeye akiwa kama captain ya club hyo

KOCHA WA STARS ATANGAZA KIKOSI CHA COSAFA

Kocha Mkuu wa timu ya Tanzania ‘Taifa Stars’, Salum Shabani Mayanga,  Jumatano Juni 14, 2017 ametangaza majina ya wachezaji 22 watakaounda kikosi kinachokwenda kushindana kuwania Kombe la Castle Cosafa nchini Afrika Kusini. Taifa Stars inayodhaminiwa na Bia ya Serengeti, inatarajiwa kuanza kambi rasmi kesho Jumapili Juni 18, mwaka huu. Kambi hiyo itakuwa kwenye Hoteli ya Urban Rose, iliyoko Mtaa wa Jamhuri katikati ya jiji la Dar es Salaam. Taifa Stars inajiandaa na michuano ya Cosafa inayotarajiwa kuanza Juni 25, mwaka huu. Michuano hiyo, inaandaliwa na Baraza la Mpira wa Miguu la nchi za Kusini mwa Afrika ambako Tanzania – mwanachama wa Cecafa, imepata mwaliko kushiriki. Tanzania imepangwa kundi A ambako wapinzani wake ni Mauritius, Malawi na Angola wakati Kundi B ni Msumbiji, Shelisheli, Madagascar na Zimbabwe. Timu za Botswana, Zambia na Afrika Kusini kadhalika Namibia, Lesotho na Swaziland zitakuwa na mechi maalumu (play off) ili kuingia robo fainali. Kwa mujibu wa Mayanga...

JEZI YA NYUMBANI YA BARCELONA MSIMU WA 2018/2019 IMEVUJA MTANDAONI

Hamza matwany Jezi ya barcelona ya msimu wa 18/19 ambayo inatengezwa na kampuni ya vifaa vya michezo vya nike imevuja mtandaoni. Jezi hiyo ambayo inafanana na jezi ambayo ilitumiwa na club hiyo mwaka 1998 miaka 20  nyuma imetengezwa katika namna hiyo ili kuenzi legends kwa klabu hiyo Jezi ya nyumbani itakuwa ina wekundu na mistari ya blue na bukta nyeusi pia socks zake ni nyeusi kama inavyoonekana kwenye hizo picha