Skip to main content

Posts

Showing posts from January, 2018

TATHMINI KUELEKEA DAR DERBY AZAM VS YANGA SC.

Hamza matwany Weekend hii kutakuwa na kati ya zile mechi kubwa kwenye vodacom premier league( vpl) kati ya wenyeji azam fc mabingwa wa afrika mashariki na kati ikikutana na mabingwa wa kihistoria wa ligi hyo yanga sc. Ushindani wa yanga na azam unatenganishwa na goli moja na ushindi wa mechi moja kati yao Yanga na azam zimekutana mara 18 kwenye vpl tangu zilipokutana kwa mara kwanza mwaka 2008 katika mechi hizo yanga amefanikiwa kushinda mechi 6 na azam ameshinda mara 5 huku wakitoka sare michezo 7. Katika mechi hizo yanga amefunga magoli 26 na azam amefunga magoli 25. Kwenye mashindano yote ambayo azam na yanga wamekutana takwimu zao ni kama ifuatavyo; Wamekutana mara 31 yanga ameshinda mara 12 na azam ameshinda mara 11 huku wakiwa wametoka sare mara 8. Huku yanga akiifunga magoli 41 na azam fc wakiwa wamefunga magoli 40. UBORA WA VIKOSI VYAO KWA SASA Kwa msimu huu azam amekuwa na matokeo mazuri katika vpl akiwa ajapoteza mchezo hata mmoja wa ligi na yupo nafasi ya pili katik...

JE WAJUA?

Hamza matwany Ahn jung-hwan raia wa korea kusini alifunga goli la dhahabu kwenye dakika 30 za nyongeza kwenye kombe la dunia mwaka 2002 kwenye mchezo 16 bora dhidi ya italy, wakati huo alikuwa akicheza katika klabu ya perugia iliyopo seria B ya nchini italia. Baada ya goli hilo klabu hiyo iliamua kumvunjia mkataba mchezaji huyo

MAJERAHA MAKUBWA LIGI 5 KUBWA BARANI ULAYA

Hamza matwany Hivi unawajua wachezaji waliowahi kupata majeraha makubwa na kukaa nje siku nyingi pia kukosa michezo mingi kwenye vilabu vyao? Nmekuletea hizi takwimu za wachezaji wa ligi kubwa 5 barani ulaya kwa idadi ya majeraha waliyoyapata, siku walizokaa mpaka kupona hayo majeraha yote na michezo pia ambayo wameikosa. Premier league( EPL) Kwa upande wa ligi kuu kijana mwenye kipaji kikubwa raia wa uingereza na klabu ya arsenal Jack wilshere ndio anaongoza kwenye ligi hii akiwa amepata majeraha mara 13 akiwa ametumia siku 1013 kuuguza majeraha hayo yote .Jack wilshere amekosa michezo 155 mpaka sasa kipindi chote alichoapata majeraha hayo. La liga (santander) Kwenye ligi hii Thomas vermalein mchezaji wa fc barcelona pamoja na taifa ya ubelgiji ndio anaeongoza kwa majeraha mengi kwenye ligi hii akiwa ameumia mara 23 akiwa ametumia siku 1026 katika kuuguza majeraha yote ambayo ameyapata akiwa amekosa michezo 128 katika kipind chote cha majeraha. Bundersliga Kwenye ligi kuu uj...

PAUL POGBA AWEKA REKODI LIGI 5 BORA BARANI ULAYA

Hamza matwany Kiungo wa manchester united paul pogba ambae alichaguliwa kuwa man of the match katika mechi ambayo manchester united walicheza nyumbani dhidi ya stoke city Katika mchezo huo manchester united walishinda goli 3_ 0 magoli ya antonio valencia, martial,na lukaku na kuwafanya manchester united kurudisha matumaini ya mbio za ubingwa baada ya kubakiza point 12 na kinara wa ligi hiyo Paul pogba alichangia upatikanaji wa magoli 2 kati ya hayo matatu na kumfanya afikishe assist 9 kwenye michezo 13 ya ligi. Hivyo pogba anakuwa ame leta msaada wa mabao 9 kwenye mechi 13 ambazo ni nyingi kulinganisha na mechi ambazo amecheza kuliko wote ambao wamefanya hivyo katika ligi 5 bora barani ulaya kwa sasa. Takwimu Pogba 9 kwenye mechi 13 Neymar 9 kwenye mechi 14 Phili max 9 kwenye mechi 18 Sisto 9 kwenye mechi 19 Leroy sane 9 kwenye mechi 21 Kelvin de bruyne 9 kwenye mechi 23

DEMBELE OUT WIKI 4

Hamza matwany Madaktari wa klabu ya barcelona wamethibitisha osmanè dembele raia wa ufaransa atakuwa nje kwa wiki 3 hadi 4 kutokana na majeraha ya msuli ambayo aliyapata kwenye mechi dhidi ya real socieded kwenye uwanja wa anoeta jumapili Mchezaji huyo akiwa ametoka kwenye majeraha ya muda mrefu baada ya kukaa nje kwa miezi minne tangu alipoumia mwezi wa nane kwenye mechi dhidi ya getafe. Madaktari wa klabu wamethibitisha majeraha hayo hayata athiri lile jeraha lake la kwanza la upasuaji alilofanya mwezi wa 8 Bado osmane dembele ajakuwa na wakati mzuri kutokana na majehara hayo yanamsumbua.

JEZI YA NYUMBANI YA BARCELONA MSIMU WA 2018/2019 IMEVUJA MTANDAONI

Hamza matwany Jezi ya barcelona ya msimu wa 18/19 ambayo inatengezwa na kampuni ya vifaa vya michezo vya nike imevuja mtandaoni. Jezi hiyo ambayo inafanana na jezi ambayo ilitumiwa na club hiyo mwaka 1998 miaka 20  nyuma imetengezwa katika namna hiyo ili kuenzi legends kwa klabu hiyo Jezi ya nyumbani itakuwa ina wekundu na mistari ya blue na bukta nyeusi pia socks zake ni nyeusi kama inavyoonekana kwenye hizo picha

MACHACHE KUELEKEA MCHEZO WA REAL SOCIEDED DHIDI YA BARCELONA

Hamza matwany Kuelekea mchezo wa real socieded dhidi ya barcelona leo katika uwanja wa nyumbani wa real socieded Anoeta stadium, hizi ni takwimu chache kabla ya mchezo huo Barcelona wanaongoza ligi kwa point 48 huku real socieded wakiwa nafasi ya 13 kwa point 23 katika michezo 18. Kwenye mechi 7 za mwisho za la liga katika uwanja wa anoeta barcelona hawajawahi kushinda mchezo hata mmoja kati ya hiyo wamefungwa michezo 5 na kutoa sare mara mbili. Mara ya mwisho barcelona kumfunga real socieded katika uwanja wake wa nyumbani ilikuwa mwaka 2007 katika ushindi wa goli 2_0 Mpaka sasa kwenye mechi 6 za mwisho za ligi real socieded ajashinda mchezo wowote amefungwa michezo 3 na kutoa sare michezo 3 msimu huu Barcelona hajaruhusu goli lolote katika mechi zake 4 za mwisho za laliga msimu huu mara ya mwisho kufanya hivyo ilikuwa may 2016. Real socieded  wamefunga magoli 6 katika dakika 15 za mwanzo kwenye la liga msimu huu. Messi ndo kinara wa magoli kwenye mechi hii akiwa amefung...

MANENO YA TON KROOS BAADA YA KUFUNGWA NA VIRAREAL

Hamza matwany Baada ya mchezo wa real madrid dhidi ya mbweha wa spain virareal katika uwanja wa sentiago bernabeu na mchezo kumalizika kwa madrid kufungwa goli moja katika dakika ya 88 ya mchezo. Kufuatia matokeo hayo madrid wanakuwa wameachwa point 16 dhidi ya mahasimu wao wa el classico fc barcelona ambao wanaongoza ligi hyo kwa sasa. Real madrid ipo nafasi ya nne baada ya kucheza 18 wakipata point 32 wakiwa mbele kwa point moja tu na timu ambayo ipo nafasi ya tano virareal na ikiwa point 3 mbele dhidi ya timu ambayo ipo nafasi ya 6 Baada ya kupoteza mchezo huo haya ndio yalikuwa maneno ya kiungo kwa kijerumani katika mahojiano ton kroos "Tumepoteza mchezo na tupo nyuma kwa point 16 dhidi ya klabu ambayo inaongoza ligi kilichobaki kwa sasa ni kuhakikisha klabu inafuzu kwa mashindano ya ulaya mwakani kuwania ubingwa kwa msimu huu kama imekuwa ngumu sana kwa upande wetu"

ARDA TURAN NA MAISHA MAPYA YA SOCCER

Hamza matwany Klabu ya barcelona rasmi imemuachia mchezaji wake arda turan kwa mkopo kwenye klabu ya Bà sà k séhīr ya nchini uturuki. Arda turan  30 atakuwa kwa mkopo wa miaka 2 na nusu  katika klabu hiyo na baada ya hapo barcelona wanaweza kumuuza kwenye klabu yoyote ya ulaya na pia kwenye mkataba wake wa mkopo kuna kipengele cha mkopo ambacho kinawaruhusu instabul basaksehir kumnunua kwa jumla baada ya muda huo wa mkopo    na rasmi jana ametambulishwa kwenye klabu hiyo ya uturuki. Barca walimnunua arda turan kutoka atletico madrid akiwa kwenye kiwango kizuri sana lakini mambo hayakumuendea sawa akiwa na fc barcelona Arda turan aliandamwa na majeruhi ya muda mrefu katika club hiyo hali iliyomfanya akose nafasi ya kucheza katika klabu hiyo. Arda turan amedumu  katika ligi kuu spain kwa misimu sita na ameshinda la liga, europa league . Alijiunga na atletico madrid akitokea klabu ya galatasaray ya nchini kwao uturuki, pia likiwa zao ya galatasaray youth acad...

WANAWAKE WATAZAMA MECHI KWA MARA YA KWANZA

Hamza matwany Wanawake saudi arabia kuangalia mpira kwa mara ya kwanza nchini humo. Wanawake hao kwa mara ya kwanza wameruhusiwa kutazama mechi kati ya al _ ahr kwenye uwanja wake wa nyumbani ambao walikuwa wanacheza mchezo wa ligi dhidi ya al _ batin Zamani sheria za saudi arabia zilikuwa haziruhusu wanawake kwenda uwanjani kushuhudia mchezo lakini baada ya kubadilisha sheria hiyo kwa sasa wanawake wapo huru kushuhudia michezo mbalibali ya soccer MABADILIKO

JUVENTUS NA MIPANGO YA ZIDANE

Hamza matwany Zinedine zidane huenda akawa kocha mrithi wa massimiliano allegri hapo mwezi juni katika club ya juventus. Massimiliano amekuwa akitajwa na vlabu kama chelsea, arsenal,kwenda kuchukua mikoba ya makocha wanaoziongoza timu hizo kwa sasa. Katika kura zilizopigwa na uongozi wa juventus zidane ndo ameongoza na huenda akawa mrithi wa massimiliano allegri. Zidane kwa sasa ambae hana msimu mzuri mwaka huu na club yake ya real madrid na madrid huenda wakatafuta mbadala wa kocha huyo kwenye dirisha kubwa la usajili wa mwezi juni. Huku kocha wa totnham hotspurs pochett ino ikiripotiwa kuwa mbadala wa zidane.

PEP GURDIOLA AVUNJA REKODI EPL

Hamza matwany Kocha mkuu wa manchester city pep gurdiola aweka rekodi mpya katika ligi kuu ya england( epl ) . Pep gurdiola ameweka rekodi hiyo baada ya kuchukua tuzo nne mwezi September October November December Pep gurdiola anakuwa manager wa kwanza wa epl kuweka rekodi hiyo  baada ya hapo mwanzo kuwekwa na antonio konte kocha mkuu wa chelsea kwa kuchukua mara tatu mfululizo. Pep amechukua tuzo ya mwezi december baada ya kucheza michezo saba( 7 ) ya ligi kuu na kushinda michezo sita na kutoa sare mchezo mmoja dhidi ya crystal palace. Pep anaungana na harry kane ambae amechukua tuzo ya mchezaji bora epl mwezi december kwa kufunga ha_trick tatu katika mwezi huo Pia goli bora la mwezi december limefunga na jerman defoe wa fc bounamouth goli ambalo alifunga dhidi ya crystal palace.

GOLI TATA LA DONALD NGOMA DHIDI YA LIPULI